Mitazamo kuhusu lugha ya kiswahili
wataalamu hudai kuwa asili ya lugha ya Kiswahili ni huko Kongo ambayo baadaye iliitwa Zaire na sasa inaitwa Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo. Dai hili linaimarishwa na wazo lingine linalodai kwamba katika vipindi kongwe vilivyopat kuwako, sehemu za Pwani ya Afrika mashariki hazikuwa zimekaliwa na watu. Kutokana na hali ya vita, uchungaji na biashara, inadaiwa kuwa Wabantu walitoka sehemu za Kongo walisambaa na kuja pwani ya Afrika mashariki kupitia Kigoma. Baadhi ya wabantu hawa walipitia sehemu za Uganda. Wakati wa kusambaa kwao, walieneza pia lugha zao ikiwemo hii ya Kiswahili.
Udhaifu wa nadharia hii ni kwamba, madai ya kuwa asili ya Kiswahili ni Kongo hayana msingi kwani mpaka sasa wataalamu wanaodai hivi hawajaweza kueleza na kuthibitisha kisayansi ama Kihistoria juu ya lini hasa watu walianza kuishi pwani ya Afrika mashariki.
Kiswahili ni Ki-Pijini au ni Ki-Krioli
(i) Kiswahili ni Ki-Pijini
Baadhi ya wataalamu hudai kuwa Kiswahili ni Ki-Pijini. Wataalamu hawa hudai kwamba Ki-Pijini ni lugha ambayo huzaliwa kutokana na kukutanika kwa makundi mawili (A) na (B) yanayotumia lugha mbili tofauti. Ili makundi haya yaweze kuwasiliana kunaundwa lugha ambayo kitabia ni tofauti na zile zinazozungumzwa na makundi yanayohusika. Lugha hii inaweza kuwa na msamiati mwingi kutoka lugha kati ya zil mbili, au inaweza kuwa na msamiati wenye uzito sawa. Lugha hiyo ndiyo inayoitwa Ki-Pijini. Mazingira yanayosababisha kuwepo Ki-Pijini ni kam vile biashara, utumwa, ukoloni, nk.
Kwa mantiki ya nadharia hii, wataalamu hawa hukiona Kiswahili kuwa kilianza kama Ki-Pijini kwani ni tokeo la mwingiliano baina ya wenyeji wa pwani y Afrika Mashariki na wageni wa kutoka Mashariki ya Kati, hususan Waarabu. Aidha, husisitiza kuwa lugha ya Kiswahili haikuwepo kabla ya hapo.
(ii) Kiswahili ni Ki-Krioli
Wataalamu hawa wanadai kwamba watu wanaozungumza Ki- Pijini wanaweza kuishi pamoja kwa muda wa karne nyingi na kwa hiyo wakaweza kuzoeana na hata kufikia hatua ya kuoana. Wakioana watot wao huikuta lugha ya ki-Pijini ama lugha yao ya kwanza. Inapofikia hatua ya aina hii kwa watoto wanaozungumza lugha hiyo, wao husemekana sasa
wanazungumza lugha ya Ki-Krioli, lugha ambayo ni hatua ya juu ya Ki-Pijini, yaani Ki-Pijini kilichokomaa.
Nadharia hii hutumia kigezo cha msamia wa Kiswahili kuonesha uhusiano uliopo kati ya Kiswahili na Kiarabu. Wanadai kuwa, msamiati mwingi wa Kiswahili unatokana na Kiarabu. Hivyo huhitimisha kuwa hapana shaka Kiarabu kimehusika katika kuizalisha na kuikomaza lugha ya Kiswahili.
Udhaifu wa nadharia hii ni kwamba hutumia kigezo cha msamiati tu bila kuzingatia vipengele vingine vya lugha kama vile matamshi, maumbo ya manen au muundo wa sentensi za Kiswahili. Aidha, wataalamu hawa hawakuhoji sual la kufanana kwa Kiswahili na lugha jirani katika hayo yaliyotajwa hapo juu na katik eneo la Kijografia ambamo Kiswahili na lugha hizo nyingine hujikuta zikizungumzwa. Vigezo hivi ni ushahidi tosha unaoonesha kuwa Kiswahili SI Ki-Pijini wala SI Ki-Krioli, bali ni lugha kama zilivyo hizo lugha jirani.
Kiswahili ni Lugha ya Jamii ya Vizalia
Kundi la kwanza la wataalamu wa nadharia hii, Bishop Edward Steera, Bwana Taylor, Dkt. R. Reusch, (Katika Maganga, 1997) hudai kwamba:
· Waarabu na Waajemi waliohamia pwani ya Afrika ya Mashariki waliwao wanawake wa ki-Afrika.
· Watoto wao walijifunza maneno y Kiarabu na ki-Ajemi kutoka kwa baba
· Aidha, watoto hao wakajifunza maneno ya ki-Bantu kutoka kwa mam zao.
· Katika jitihada zao, watoto hao walijirekebisha kutokana na tamadun wazazi wao ambazo ni tafauti: utama wa Kiarabu na utamaduni wa ki-Bant
· Vizalia hawa wakaanza kutumia lu mpya ya mseto wa Kiarabu, Kiajemi n lahaja mbalimbali za ki-Bantu.
· Kwa kiasi kikubwa, lugha mpya ya mseto ilikuwa ni upotoshaji wa lugha Kiarabu na Kiajemi.
· Mwarabu au Mu-Ajemi alikuwa muumini wa dini ya Uislamu.
· Umo humo, vizalia hawa wakayain maneno ya Kiarabu, Kishirazi na Kihin katika hii lugha mpya.
· Pamoja na kuyaingiza maneno ya kigeni, lugha-mpya yao hii (Kiswahili), ilikithiri vionjo vingi vya lugha mbali za ki-Bantu.
· Ndipo baadaye, lughampya yao hii ikajulikana au kuitwa Kiswahili.
· Kwa maoni ya wataalamu hawa, sehemu mbili kati ya tano (2/5) ya maneno yanayotumika katika lugha hi mpya ni ya ki-Bantu.
· Sarufi ya lugha mpya hii ni mseto ki-Bantu (chenye utata na kisicho na mpangilio maalumu) pamoja na Kiara (chenye mantiki na kilichokomaa).
Kundi la pili la wataalamu wa nadharia hi B. Krumm na F. Johnson lina mawazo yanayodai kwamba:
· Kiswahili kilitokana na visiwa vya Lamu, Kilamu/Kiamu.
· Wageni kutoka Ghuba ya Ushirazi/Uajemi na Arabia ya Kusini walikuja k Pwani ya Afrika ya Mashariki na lugha tofauti.
· Lakini kutokana na kuoana kwao wenyeji, wageni hawa wakaichukua lu ya hapo walipofikia, wakaikuza kwa maneno kadhaa na sentensi kadhaa kutoka lugha zao za asili, yaani Kiara Kiajemi na Kihindi hususan katika masuala ya biashara, ubaharia, vyom vya kazi zao na nguo.
· Aidha, utumwa na tabia ya kuoa wengi ilisaidia kutoa kundi kubwa la masuria. Hali hii ikaondosha hisia za ugeni katika lugha zao; na maneno y yakabatizwa kuwa ya ki-Bantu, na hat kupoteza kabisa sura ya ugeni.
Kiswahili ni Kiarabu
Kuna hoja kuu tatu ambazo baadhi ya wananadharia hii huzitumia kutetea nadharia hii kuwa Kiswahili asili yake ni Kiarabu.
(i) Inadaiwa kuwa maneno yenye a Kiarabu yaliyomo katika Kiswahili ni tosha kwamba lugha hii ilianza kam Pijini ya Kiarabu.
(ii) Inahusu neno lenyewe Kiswahili asili yake ni Kiarabu. Neno Kiswahili linatokana na neno “sahili” (umoja) “swahil” (wingi) lina maana ya pwan
(iii) Inadaiwa kwamba kwa kuwa Kisw kilianza pwani, kwa kuwa idadi kub sana ya wenyeji wa pwani ni waisla kwa kuwa uisilamu uliletwa na Waar basi Kiswahili nacho kililetwa na W
Kiswahili si Kiarabu
Madai kwamba Kiswahili si Kiarabu yanathibitishwa na hoja kinzani zifuatazo
Tukianza na dai la kwanza ‘kwamba maneno yenye asili ya Kiarabu yaliyomo katika Kiswahili ni ishara tosha kwamba lugha hii ilianza kama pijini ya Kiarabu’ tunaona wazi kwamba madai haya hayan mashiko. Lugha ya Kiswahili imetokea kuwa na maneno ya mkopo yenye asili ya Kiarabu (na kwa hakika yapo yenye asili y Kiajemi, Kireno, Kihindi, Kijerumani, Kiingereza nk.) kutokana na ukweli kwamba kulikuwa na mawasiliano ya karne na karne baina ya wenyeji wa pwan na wafanyabiashara wa Kiarabu. Wasemaji wa lugha mbili tofauti wanapokutana hawaachi kuathiriana kilugha. Kwa hiyo lugha kuwa na maneno mengi ya mkopo kutoka lugha nyingine, haifanyi lugha hiyo isemekane kuwa imetokana na hiyo lugha nyingine.
Pili wataalamu hawa wanadai kwamba neno lenyewe Kiswahili lina maana ya Kiarabu.
Kwani linatokana na neno “sahili” (umoja na “swahil” (wingi) lina maana ya pwani. Hapa ingetupasa tuelewe kwamba kila mtu binafsi au jamii binafsi aghalabu hajiiti mwenyewe jina lake, yeye huitwa kwa hilo jina alilopewa na wengine: Jamii yake au wageni waliomtembelea kwake. Na hivi ndivyo ilivyojitokeza kwa upande wa jamii ya watu wa pwani ya Afrika mashariki, yaani Waswahili,
walipotembelewa na Waarabu na kuitwa As-Sahilyy au As-Sawahiliyy, na nchi yao kuitwa sahil (wingi wake Sawahil), yaani pwani (upwa), ufuo. Kwa mantiki hii, dai hili halina mashiko !
Kigezo cha dini nacho hakikubaliki lugha haiwi lugha kwa sababu ya imani. Hata hivyo lugha ya Kiarabu yenyewe ilikuwep karne nyingi kabla ya kufunuliwa dini ya Uislamu. Hali kadhalika, lugha nyingine z Kimagharibi zilikuwepo karne nyingi kabl ya kufunuliwa imani ya ukristo. Kama ilivyo kwamba Kiingereza au Kijerumani s ukristo, basi ndivyo vivi hivyo ilivyo kwamba Kiswahili hakiwezi kuwa dini ya uislamu, aslan! Wala Kiarabu nacho si uislamu. Tunachoweza kufanya ni kuitumia lugha kuifasili dini, lakini hatuwezi kuitumia dini kuifasili lugha.
Kiswahili ni Kibantu
Vipengele vinavyotumika katika kuihalalisha nadharia inayodai kwamba Kiswahili ni Kibantu ni ushahidi wa ki-Isimu, ushahidi wa ki-Historia na kuichunguza lugha ya Kiswahili katika mfumo mzima wa historia ya mgawanyik wa kusambaa kwa lugha za ki-Bantu. Wataalamu wa nadharia hii wanahitimish kwa kudai kwamba Kiswahili ni mojawap kati ya lugha katika jamii kubwa ya lugha za ki-Bantu.
Baadhi ya wataalamu muhimu wanaoiunga mkono nadharia hii ni Prof. Malcon Guthrie, Dkt. C. Meinholf na Dkt. C. Rohl na Prof. Clement Maganga.
Profesa Malcom Guthrie ni mtaalamu (mwanaisimu) mashuhuri kutoka Chuo Kikuu cha London, Uingereza. Alitumia miaka 20 kuchunguza uhusiano uliopo baina ya lugha za Kibantu zilizoko katika eneo lote ambalo hukaliwa na wabantu. Sehemu hii ni ile ambayo inajulikana kama Afrika, Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Alifanya uchunguzi wa mashina/mizizi (viini) ya maneno 22,000 kutoka lugha 20 za Kibantu. Katika uchunguzi wake alikut mizizi (mashina) 2,300 imezagaa
katika lugha mbalimbali za Kibantu na Kiswahili kikiwemo. Mashina/mizizi 500
yalilingana katika lugha zote 200. Mashina haya yalipatikana katika lugha zote za Kibantu. Mashina haya yalikuwa ya asili moja. Baadhi ya lugha hizo 200 zilizofanyiwa uchunguzi Kiswahili kilionesha kuitikia ulinganifu sawa na Kikongo kwa asilimia arubaini na nne (44%).
Katika kuchunguza ni asilimia ngapi za mashina hayo 500 yaliyomo katika kila lugha, mgawo uliojitokeza ulikuwa kama ifuatavyo:
Kiwemba kizungumzwacho Zambia -
54%
Kiluba kizungumzwacho Katanga -
51%
**Kikongo kizungumzwacho Zaire -
44%**
**Kiswahili kizungumzwacho Afrika Mashariki 44%**
Kisukuma kizungumzwacho Tanzania 41%
Kiyao kizungumzwacho Tanzania/Msumbiji - 35%
Sotho kizungumzwacho Botswana - 20%
*Kirundi kizungumzwacho Burundi -
43%*
Kinyoro kizungumzwacho Uganda -
37%
Kizulu kizungumzwacho Afrika Kusini -
29%
Baada ya kupata matokeo haya, Profesa Malcom Guthrie anaiunga mkono nadharia hii ya kwamba Kiswahili ni ki-Bantu kwa kudai kwamba:
(i) Kiswahili kilikuwepo kabla ya ujio w wageni;
(ii) Anaonyesha kwamba Kiswahili kina uhusiano mkubwa na lugha za Kiba
(iii) Mwisho anasema Kiswahili kilianzia ya Afrika Mashariki.
Dkt. C. Meinholf na Dkt. C. Rohl: Wataalamu hawa wanaamini kwamba:
(i) Wakati wa utawala wa Shir katika upwa wa mashariki ya Afrik kulikuwa na kabila la Waswahili;
(ii) Kabila hili ni dhuria ya Wazar leo.
(iii) Kwa kuwa hawa Wazaramo w wamezaliwa katika harakati za kib kwa hivyo wakafuata nyayo za wa wao.
(iv) Lugha yao ilikuwa ya aina ya
(v) Kwa kuwa Wabantu ni wengi kuliko jamii ya makabila mengine, yao ya Kiswahili ikaanza kutumika kuenea katika makabila mengine, katika ukanda wa pwani ya Afrika Mashariki.
(vi) Baadaye, Waswahili hawa ha wakafanya biashara na wageni wa kuvinjari Afrika Mashariki, hususa Waarabu, Washirazi, Wamalaysia, na Wareno ambao tayari walikuw wamefurika katika pwani hii ya Afr Mashariki miaka kadhaa kabla.
(vii) Vifaa na majina ya vitu vya bia vya wageni hao vikaselelea na kui katika mfumo wa lugha hiyo ya W ambayo ni ki-Bantu.
Madai ya nadharia hii yakichunguzwa, tunagundua kwamba inazingatia mitazamo miwili yaani, mtazamo wa ki-Isimu na mtazamo wa ki-Historia. Kwa mantiki hii, nadharia hii inaelekea kukubalika na wataalamu wengi kuwa ndiyo sahihi kuhusu asili au historia ya Kiswahili.
Profesa C. Maganga, na uthibitisho wake kwamba Kiswahili ni ki-Bantu. Kama tulivyoona, lugha ya Kiswahili ilifanyiwa utafiti na uchambuzi na wanataaluma kadhaa kwa madhumuni ya kuiainisha kama ilikuwa yenye misingi ya ki-Bantu a la. Prof. Maganga alifanya uchambuzi wa ki-Isimu na wa ki-Historia kuhusu lugha hii. Matokeo ya utafiti wake wa ki-Isimu kuhusu lugha ya Kiswhili (au lugha kwa ujumla) unadhihirisha mambo mengi, mojawapo ni asili ya lugha hiyo. Amethibitisha kwamba Kiswahili ni lugha ya Kibantu; na kwa hivyo, kuthibitisha kw ushahidi thabiti hoja ya Dkt. C. Meinholf na Dkt. C. Rohl kama tulivyoieleza hapo juu.
(i) Ushahidi wa Kiisimu
(a) Msamiati
Matokeo ya utafiti alioufanya kuhusu msamiati wa Kiswahili ulibaini kwamba 60% ya maneno yote yanayoweza kuandikwa na kutamkika katika lugha ya Kiswahili asili yake ni lugha za Kibantu, 30% ni lugha ya Kiarabu na 10% ni lugha nyingine za kigeni kama vile Kiingereza, Kireno, Kijerumani, Kihindi, Kiajemi, Kifaransa, nk. Kinyume chake ni kwamba msamiati wa Kiswahili na ule wa Kibantu hautofautiani.
Mfano:
Kiswahili Kindali Kizigua Kijita
Kikurya Kindendeule
Mtu Umundu Mntu
Omun Omontu Mundu
Maji Amashi Manzi
Amanji Amanche Maache
Moto Umulilo Moto
Omulilo Omoro Mwoto
(b) Tungo (Sentesi) za Kiswahili
Miundo ya tungo (sentesi) za maneno ya Kiswahili zinafanana sana na miundo ya tungo za maneno ya ki-Bantu. Sentesi za Kiswahili na za lugha za ki-Bantu zina kiima na kiarifu.
Mfano:
Lugha za Kibantu
Kiima kiarifu
Kiswahili
Juma anakula ugali.
Kizigua
Juma adya ugali.
Kisukuma
Juma alelya bugali
Kindali
Juma akulya
ubbugali.
Kijita
Juma kalya ubusima.
Kindendeule
Juma ilye ughale.
(c) Ngeli za Majina
Wanataalamu wanakubaliana kuhusu nge za majina kwa mujibu wa:
maumbo ya nomino (umoja na wingi wa majina) pamoja; na
upatanisho wa kisarufi katika sentesi.
Kigezo cha maumbo ya majina: Kigezo hiki hufuata maumbo ya umoja na uwingi katika kuyaainisha majina. Majina yaliyo mengi katika lugha ya Kiswahili na lugha za ki-Bantu hufuata mkondo wa umoja n uwingi. Majina ya lugha ya Kiswahili na lugha za ki-Bantu yaliyo mengi yana maumbo dhahiri ya umoja na uwingi.
Mfano:
Lugha za Kibantu
Umoja Wingi
Kiswahili mtu
watu
mtoto
- watoto
Kikurya omanto
- banto (abanto)
omona - bana
(abana)
Kizigua mntu
bhantu
mwana
- bhana
Kindali mundu
- bhandu
mwana
- bhana
Kindendeule mundu
βhandu
mwana
- βhana
Kigezo cha upatanisho wa kisarufi katika sentesi: Katika kigezo hiki tunaangalia uhusiano uliopo kati ya kiima (jina na viambishi awali vya nafsi) na vivumishi katika vitenzi vya Kiswahili na ki-Bantu. Vivumishi, majina pamoja na viambishi hivyo vya vitenzi hubadilika kutokana na maumbo ya umoja na uwingi.
Mfano:
Lugha za Kibantu Umoja -
Wingi
Kiswahili Baba analima
Baba wanalima
Kindali Utata akulima
Abbatata bbakulima
Kikurya Tata ararema
Batata(Tata)bararema
Kijita Tata kalima - Batat abalima
Kindendeule Tate ilima
Akatate βhilima
(d) Vitenzi vya Kiswahili na Kibantu
Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya vitenzi vya Kiswahili na vile vya lugha zingine za ki-Bantu. Vipengele vinavyothibitisha uhusiano huu ni: Viambishi, mnyumbuliko, pamoja na mwanzo au mwisho wa vitenzi, kama ifuatavyo:
Viambishi: vitenzi vya lugha ya Kiswahili na vya lugha zingine za ki-Bantu hujengw na mzizi (kiini) pamoja na viambishi vyak vya awali na vya tamati.
Mfano:
Kiswahili - analima =
a – na – lim - a
Kiikuyu - arerema =
a – re – rem–a
Kindali - akulima =
a - ku – lim – a
1 - 2 - 3 - 4
Sherehe:
1 - Kiambishi awali kipatanishi cha nafsi.
2 - Kiambishi awali cha njeo (wakati uliopo).
3 - Mzizi/Kiini.
4 - Kiambishi tamati.
Mnyambuliko wa vitenzi: Mnyumbuliko w vitenzi vya Kiswahili hufanana na ule wa vitenzi vya lugha za ki-Bantu.
Mfano:
Kiswahili - kucheka -
kuchekesha - kuchekelea.
Kindali - kuseka -
kusekasha - kusekelela.
Kibena - kuheka -
kuhekesha - kuhekelea.
Kinyamwezi - kuseka -
kusekasha - kusekelela.
Kikagulu - kuseka -
kusekesha - kusekelela
Mwanzo wa vitenzi: Vitenzi vyote vya Kiswahili na vile vya lugha za ki-Bantu huanza na viambishi ambavyo ni viwakilishi vya nafsi, kama ifuatavyo:
Mfano:
Kiswahili - N i-nakwenda
Kihaya - Ni-ngenda
Kiyao - N- gwenda
Kindendeule - Ni- yenda
Mwishilizo wa vitenzi: Vitenzi vya lugha za ki-Bantu na Kiswahili huishia na irabu –a.
Mfano:
Kiswahili kukimbi-a - kuwinda - kushuk-a
Kindali kukind-a -
kubhing-a - kukol-a
Kisukuma kupil-a -
kuhwim-a - Kutend-a
Kisunza kwihuk-a - kuhig-a - kising-a
Kindendeule kuβhutuk-a -
kuhwim-a - kuhuk-a
tafiti wa Prof. Maganga kuhusu ushahidi wa ki-Isimu wa kuthibitisha kama Kiswahili ni ki-Bantu au la ungeweza kuelezwa kimuhtasari kwa mifano mingine ifuatayo:
Mfano wa 1:
Lugha Se
Kiswahili
Kipare
Kindamba
Kichaga
Kihaya
Kikaguru
Kindendeule
Jongo
Jongo
Jongo
Jongo
Jongo
Jongo
Jongo
anafuga
erisha
kafugha
nao he
n’afuga
kachima
ifuga
mbuz
mbuji
mene
mbur
embu
m’eh
mbuh
Katika mfano huu inaonekana kwamba mpangilio wa maneno katika sentesi una ufanano kwa sababu katika kila sentesi kuna kiima na kiarifu. Katika kiima kuna nomino, yaani jina la mtenda (Jongo) na katika kiarifu kuna kitendo kinachofanyik na nomino mtendwa. Pia nafasi ya viunganishi ni ile ile kwa lugha zote zilizoonyeshwa katika mfano huu.
Kuna mfano mwingine wa ufanano wa mpangilio huu.
Mfano wa 2:
Lugha Sente
Kiswahili
Kihaya
Kisukuma
Kinyaturu
Kipare
Kizigua
Sitamkuta kesho
Timushangemu n
Natusanga inton
Tumuhanga fady
Nesikemkiche ya
Sirambila luvi
Katika sentensi hizo mpangilio wa maneno una ufanano kwa sababu kila sentensi ina kiima na kiarifu chenye kitenzi na kielezi. Pia kiambishi cha nafsi cha nomino ya mtenda kinajitokeza mwanzoni mwa neno la kwanza la kila sentesi.
Si tamkuta; Ti mushangemu;
Natusanga;
Tu muhanga;
Nesikamkiche; Si tambila.
Viambishi hivyo vya nafsi ya mtenda pia vinaonyesha hali ya ukanushi katka kila sentesi na nafasi yake ni ile ile kwa kila sentesi.
Viambishi vya urejeshi navyo vinajitokeza katika kitenzi cha kila sentesi.
Viambishi {m}, {m}, {ti}, {tu} sita m kuta,
timushangemu, na tu sanga, tumuhanga, nesika m kiche, na sita m bwila ni vya urejeshi; vinawakilisha nomino mtendwa.
Kwa hivyo, hali hii inadhihirisha kwamba miundo ya sentensi hizi inafanana na vitenzi vyake vina tabia mbalimbali, kam vile:
(i) kubeba viambishi vya nafsi, mtenda na mtendwa,
(ii) kuonyeshga hali ya ukanushi njeo za wakati na kitendo kinachofanyika.
Mfano wa 3:
Lugha
Kiswahili
Kizigua
Kihaya
Kisukuma
Kinyaturu
Kipare
Kindendeule
Akija
Akez
Kalaij
Ulu n
Newa
Ekiza
Anda ango
Katika sentesi hizo inaonekana kwamba sentesi zote zinafanana kimpangilio. Pia maneno yake yanakubali uambishaji, kwa mfano:
(i) Katika maneno ya mwanzo:
akija, akeza. kalaija, akuja, newaj herufi zilizopigiwa vistari ni viamb nafsi vinawakilisha dhana ya mten
(ii) Vivyo hivyo katika maneno:
anifuate, ampondele, anitimile, an aniratere, angobhekeraye, viambis vilivyoko katika viarifu vya sentesi vinawakilisha nafsi za watenda.
(iii) Pia vitenzi vya sentesi hizo vina ta kubeba virejeshi vya nafsi kama ili katika, m wa m bie, omu gambile, na ha li, m b we le na u m ti, vinaonye na hali ya uyakinifu- hali inayoony ufanano wa maumbo ya maneno.
(iv) Licha ya kuwa na mpangilio unaof na wa lugha nyingine za kibantu, k mfano, katika mifano tuliyoiona h baadhi ya maneno yanafanana: ta maneno:
kafugha (Kindamba); nafuga
(Kihaya);
nifuga (Kindendeule); anafuga
(Kiswahili).
Pia maneno:
nkuku (Kipare); nguku (Kindamba);
nguku (Kichaga); enkoko
(Kihaya);
ng’uku (Kikaguru);
nguku(Kindendeule);
nguku (Kindendeule)
Katika mfano wa 3, maneno yafuatayo yana ufanano:
Akeza (Kizigua); kalaija
(Kihaya); alize (Kisukuma),
newaja (Kinyaturu); ekiza
(Kipare); anda ahikite,... (Kindendeule);
akija, (Kiswahili.)
Pia maneno;
umugambe (Kizigua); omugambile
(Kihaya); unongeraye (Kindendeule);
na mwambie (Kiswahili).
Ufanano huu wa msamiati, maumbo ya maneno pamoja na wa mpangilio wa maneno katika sentesi, vyote vinathibistisha kwamba lugha ya Kiswahil ni ya kibantu kama zilivyo nyingi nyinginezo.
(ii) Ushahidi wa Kihistoria Kwamba Kiswahili ni Kibantu
Baada ya kuangalia ushahidi wa kiisimu kuhusu asili ya Kiswahili, katika sehemu hii Maganga (1997) aliendelea kuchambu ushahidi wa Kihistoria unaothibitisha kuwa lugha ya Kiswahili ilizungumzwa katika upwa wa Afrika Mashariki hata kabla ya ujio wa wageni kama vile Waarabu na Wazungu. Ushahidi huu ulitolewa na wageni mbalimbali waliofika hapa Afrika Mashariki. Wote wanathibitisha kuwa lugha ya Kiswahili ilizungumzwa hapa Afrika Mashariki kabl ya ujio wa wageni.
(a) Ugunduzi wa Ali-Idris (1100-1166)
Ugunduzi huu yasemekana ulifanywa huk Sicily yapata mwaka 1100-1166. Kwenye mahakama ya mfalme Roger II. Licha ya kufahamika kuwa Kiswahili, kilipata kuandikwa kabla ya 10BK. Ali-Idris alikuwa wa kwanza kugundua jina la zamani la Zanzibar kuwa ni Unguja. Katik maelezo yake anaandika pia majina kam vile kikombe, mkono wa tembo, muriani, na kisukari, ambayo ni ya ndizi mbalimba zilizokuwa zikipatikana huko.
(b) Ushahidi wa Marco Polo
Huyu ni mzungu ambaye alijishughulisha sana na masuala mbalimbali ya kijiografi na alisafiri sehemu nyingi duniani. Marco Polo aliandika hivi:
“Zanzibari ni kisiwa kizuri ambacho kina ukubwa wa mzunguko wa maili 200. Wat wote wanaabudu (Mungu), wana Mfalme na wanatumia lugha yao, na hawalipi kod (ushuru) kwa mtu.” Safari za Marco Polo 1958:301
Marco Polo anasemekana aliandika pia kitabu cha jiografia ambacho hakikupata kuchapishwa lakini sehemu zake zimepata kufasiriwa kwa Kirusi na Kifaransa. Mfano mmojawapo ni huu unaofuata:
“Katika visiwa vya Sjawaga vilivyoshughulikiwa katika sura hii, ni kile kisiwa cha Andjaba ambacho mji wake mkuu unaitwa katika lugha ya kwao. Zanguabar/Ungudya, na wakazi wake, japokuwa ni mchanganyiko, kwa sasa wengi wao ni Waislam…chakula chao kikuu kikiwa ndizi. Kuna aina tano ambaz zinajulikana kama kundi, fili, ambazo uzito wake waweza kuwa wakia 12, Omani, Marijani, Sukari....”
Maelezo haya ya Marco Polo yanathibitisha mambo ya msingi kuhusu wakazi wa Pwani ya Afrika ya Mashariki na lugha yao; mintarafu ya dini, chakula na utamaduni wao kwa ujumla.
(c) Ushahidi wa Al-Masudi (915 BK)
Katika moja ya maandiko yake, Al-Masud anazungumzia juu ya wakazi wa mwambao ambao walijulikana kwa jina l “wazanji”. Kwa dhana hii, neno Zanzibar linatokana na Zenzibar yaani “Pwani ya Zenji”. Katika maelezo yake Al-Masudi anaonyesha kwamba Wazenji walikuwa
“Watawala Wakilimi” ambao waliaminiwa kuwa walitawala kwa nguvu za Mungu. Kuna maelezo kuwa huenda neno “wakilimi” lina maana ya “wafalme”. Al-Masudi alisisitiza katika maelezo yake kuwa Wazenji walisema lugha kwa ufasaha na walikuwa na viongozi waliowahutubia kwa lugha yao. Kutokana na neno “zenji” kuna uwezekano kuwa kabla ya majilio ya Waarabu, Kiswahili kiliitwa “Kiazania” au “Kizanji” na wageni waliofika pwani.
(d) Ushahidi wa Ki- Historia wa Mji wa Kilwa
Kimsingi habari zinazoeleza historia ya mji wa Kilwa katika karne ya 10-16BK zinataja majina ya utani kama vile:
mkoma watu, nguo nyingi, nk. ambayo walipewa Masultani wa kwanza wa Kilwa Ali Ibn Hussein na mwanae Mohamedi Ib Ali. Kutokana na habari hizi huenda lugh ya Kiswahili ilishaanza kusemwa mnamo karne ya 10 au ya 11 BK. Maelezo ya kihistoria yanaeleza juu ya Sultani aliyeitwa Talt Ibin Al Husaini ambaye alipewa jina la utani “ Hasha Hazifiki”.
(e) Utenzi wa Fumo Liyongo (13 BK) kama Ushahidi
Shairi la zamani kabisa lililopata kuandikwa la Kiswahili, linalojulikana ni lile la Utenzi wa Fumo Liyongo . Utenzi hu inasemekana uliandikwa karne ya 13BK. Kuweko kwa shairi hili kunadhihirisha kuwako kwa lugha ya Kiswahili kabla ya karne hiyo, na kwa hivyo, huenda Kiswahili kilianza kutumika kabla ya karn ya 10BK. Baadhi ya beti za utenzi wa Fumo Liyongo ni hizi zifuatazo:
Ubeti 6: Liyongo Kitamkali,
Akabalighi vijali
Akawa mtu wa kweli
Na hiba huongeya.
Ubeti 7: Kilimo kama mtukufu
Mpana sana mrefu
Majimboni yu maarufu
Watu huja kwangaliya.
Ubeti 10: Sultani pate Bwana
Papo nae akanena
Wagala mumemwona
Liyongo kiwatokeya.
(Kutoka E.A. Swahili Committee 1973)
Lugha hii ndio mfano wa lugha iliyokuwa ikitumika kunako karne ya 13BK. Ni wazi kuwa lugha hiyo ilianza kusemwa mapema kabla ya muda huo. Hoja za kihistoria inaelezea historia ya lugha ya Kiswahili toka karne ya 10BK hadi karne ya 18BK. Kutokana na ushahidi huu ni dhahiri kuwa asili ya lugha ya Kiswahili ni Wabantu wa Afrika ya Mashariki.
jiunge nasi bofya hapa ku-install application yetu swahiliform ili usisumbuke kuingia kwenye website yetu
Asante kutembelea blog yangu, karbu tena.
AY director